Tuma & Toa Pesa

AzamPesa ni ya mitandao yote. Tuma pesa  kwenda mtandao wowote kwa wote waliojisajili na AzamPesa

Toa pesa kwa mawakala wetu Nchi nzima.

Kuhusu Huduma

AzamPesa ni njia rahisi ya kuaminika ya kutuma au kutoa pesa.

Unaweza kutuma pesa kwenda mtandao wowote ule. Kwani kila mmoja anaweza kujisajili na AzamPesa kwa laini ya mtandao huo huo alionao.

Punde tuu baada ya kukamilisha usajili wako wa AzamPesa. Utakua na uwezo wa Kutuma na Kutoa Pesa kwa gharama nafuu sana.

Huduma yetu imetengenezwa kuwa huduma iliyo rahisi kutumia na inayomuwezesha mteja kulinda na kusimamia fedha zake kwa uhuru.

Jinsi Inavyofanya Kazi

KUTUMA PESA

 

  1. Piga *150*08#
  2. Chagua 1 Tuma Pesa
  3. Tuma kwenda namba ya AzamPesa
  4. Weka namba ya simu ya mpokeaji
  5. Weka kiasi
  6. Weka namba ya siri

AU

  1. Fungua App ya AzamPesa
  2. Bofya Tuma Pesa
  3. Weka namba ya mpokeaji iliyosajiliwa na AzamPesa
  4. Weka Kiasi
  5. Bofya Endelea kisha Hakiki taarifa
  6. Bofya TUMA
  7. Weka PIN, kisha Thibitisha

Jinsi Inavyofanya Kazi

KUTOA PESA

 

  1. Piga *150*08#
  2. Chagua 3 Kutoa Pesa
  3. Weka namba ya Wakala
  4. Weka kiasi
  5. Weka namba ya siri kukamilisha muamala

AU

  1. Fungua App ya AzamPesa
  2. Bofya Toa Pesa
  3. Weka namba ya wakala ya AzamPesa
  4. Weka Kiasi
  5. Bofya Endelea kisha Hakiki taarifa
  6. Bofya TOA
  7. Weka PIN, kisha Thibitisha